Diamond: Wasafi Festival ndio show namba moja nchini, huwezi kutaja muziki bila WCB ni uongo

Diamond: Wasafi Festival ndio show namba moja nchini, huwezi kutaja muziki bila WCB ni uongo
Rais wa WCB, Diamond Platnumz amedai show za Wasafi Festival ndio show namba mmoja nchini Tanzania kwa sasa kutokana na kuwakutanisha wasanii wakubwa kwa wakati mmoja.



Platnumz amedai show nyingi ambazo zinafanyika bila wasanii wa WCB ni show za kawaida kutokana na kukosa wasanii wakubwa ambao wanatoka kwenye label hiyo kubwa ya muziki.

“Kusema kweli nategemea show zote za Wasafi Festival zijaze sana kwa sababu sisi hatujaonekana kwenye mikoa kwa muda mrefu, hatujawahi kuzunguka kwenye mikoa kwa muda mrefu. Halafu uzuri wa show zetu tunachanganyika wasanii wa WCB na wasanii wengine, lakini show nyingine sisi tunakuwa hatupo. Hii ina maana hizi ndio show namba moja nchini kwa sasa, ndio show ambazo zinawakutanisha wasanii wote, show nyingine huwezi kutaja muziki bila kutaja WCB,”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad