Filamu ya Mwisho Aliyocheza Marehemu Masogange Kuzinduliwa Desemba 15

Rammy Galis Kuzindua Filamu Yake na Marehemu Masogange
Muigizaji wa Bongo movie Rammy Galis amefunguka kuhusu uzinduzi wa Movie yake mpya aliyomshirikisha marehemu Agnes Masogange ambayo anatarajia kuizindua December 15, 2018.

Rammy Galis amefunguka na kuweka wazi kuwa moja ya jambo alilolitaja kwenye movie hiyo ni Marehemu Agnes Masogange kuigiza kuhusu madawa ya kulevya.

Kwenye mahojiano aliyofanya na waandishi wa Habari Rammy amefunguka haya kuhusu filamu hiyo:

Niliamua kumshirikisha Masogange kwenye filamu hii ya hukumu lengo langu likiwa ni kumuona anafanya kazi zake katika mpangilio nilimuona ameanza kupotea katika upande wa video queen hivyo nikaamua nimuhamishie kwenye sanaa ya filamu maana niliamini anaweza na alifanya vizuri”.

Rammy amesema filamu hiyo inayotarajiwa kuzinduliwa Desemba 15, mwaka huu katika ukumbi wa Citymall jijini Dar es Salaam itakwenda kwa jina la Hukumu,ambapo amefunguka kuwa aliamua kumshirikisha Masogange lengo likiwa ni kuhakikisha anamuhamishia katika upande wa uigizaji moja kwa moja.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad