Hatimaye Cardi B Atangaza Kuachana na Offset

Hatimaye Cardi B Atangaza Kuachana na Offset
Rapper Cardi B ametangaza rasmi kuachana na mume wake Offset kupitia ukurasa wake wa Instagram leo December 5,2018 ambapo amesema kuwa yeye pamoja na Offset wamekuwa hawana maelewano mazuri kwa muda mrefu sasa.

Cardi B amesisitiza na kusema kuwa hawezi kumchukia ila atampenda Offset kama baba wa mtoto wake na pia amekua ni mtu mzuri kwake kwenye biashara na amekuwa akijaribu kutatua matatizo yaliyopo kati yao lakini imeshindikana.

Rapper Offset na Cardi B walifunga ndoa ya siri September 20,2017 na walibahatika kupata mtoto wa kike ‘Kulture’ mwezi July 2018.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad