IGP Sirro Afanya Mabadiliko Kwenye Jeshi la Polisi

IGP Sirro Afanya Mabadiliko Kwenye Jeshi la Polisi
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amembadilisha aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza kabla ya kuhamishiwa Makao Makuu ya Polisi, DCP Ahmed Msangi kuwa Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano Makao Makuu ya Jeshi la Polisi na Msemaji wa Jeshi hilo akichukua nafasi ya ACP Barnabas Mwakalukwa ambaye ameteuliwa kuwa Mnadhimu wa Polisi Mkoa wa Pwani.

Aidha, Jeshi la Polisi nchini limewataka wananchi wote kutii Sheria bila shuruti katika kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka na kusema hakuna atakayekuwa salama endapo atavunja sheria za nchi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad