Mwendokasi Iliyoua Watatu Wanzese Polisi Yakamata watu 20

Mwendokasi Iliyoua Watatu Wanzese Polisi Yakamata watu 20
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia Madereva wa bodaboda 20 kwa kuharibu basi la Mwendokasi tukio lililotokea hivi karibuni maeneo ya Manzese na kusababisha vifo vya watu kadhaa.



Akizungumza na wanahabari mapema leo, Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, amesimulia ajali hiyo iliyosababishwa na uzembe wa dereva wa bodaboda ambaye nae alipoteza maisha muda mfupi baada ya kufikishwa hospitali.



Kufuatia tukio hilo Kamanda Mambosasa ametoa onyo kwa Madereva wa bodaboda kutopita kwenye barabara ya Mwendokasi na kubainisha kuwa tayari wameshaanza operesheni ya kupambana na vitendo hivyo.



Katika hatua nyingine Kamanda Mambosasa amewataka wakazi wa mkoa wa Dar es Salaam kuchukua tahadhari kuelekea katika sherehe za krismas na kufunga mwaka ili kujiepusha na madhara yanayoweza kutokea.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad