Ulimwengu Asajiliwa na Wapinzani wa Simba

Ulimwengu Asajiliwa na Wapinzani wa Simba
Ulimwengu amesaini mkataba huo leo ambapo klabu yake hiyo ipo miongoni mwa timu 16 zilizoingia hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika sambamba na Simba SC ya Tanzania.

Usajili huu wa Ulimwengu umekuja ikiwa ni miezi miwili tu imepita tangu avunje mkataba na klabu ya Al Hilal ya Sudan ambayo hata hivyo hakuweka wazi sababu za kuvunja mkataba na timu hiyo ndani ya miezi mitatu tu.

Klabu ya JS Saoura imethibitisha usajili huo kwa kuweka picha ya Ulimwengu akiwa na mabosi wa timu hiyo akikabidhiwa jezi tayari kwa kukipiga.

Ulimwengu huenda akakutana na Simba kwenye hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika kama ilivyokuwa kwa Yanga kwenye hatua ya makundi ya kombe la shirikisho mwaka 2016 alipokuwa akichezea TP Mazembe.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad