Viporo vya Simba Vyaipa Maswali Yanga

Viporo vya Simba Vyaipa Maswali Yanga
Kitendo cha Yanga jana kucheza mchezo wake wa 15 wa Ligi Kuu Tanzania Bara huku Simba ikiwa na mechi 12, kimezua maswali mengi huku lawama za Yanga zikienda kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi (TPLB).

Hivi sasa Simba ina michezo mitatu nyuma ya Yanga kutokana na kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo Desemba 15 mwaka huu itacheza ugenini dhidi ya Nkana FC ya Zambia kabla ya kurudiana Desemba 21 Dar es Salaam.

Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera amehoji kisa cha wapinzani wao kutocheza mechi ndani ya wiki mbili baada ya wao kurudi kufuatia kucheza mechi yao ya kimataifa.

"Yanga wakati tunacheza kombe la Shirikisho tuliporudi Kenya tulicheza baada ya siku mbili Shinyanga na baada ya hapo tukaenda Mbeya baada ya siku tatu tukaenda Rwanda," alisema.

Ofisa habari wa TFF, cLIFORD Ndimbo alisema kuwa mipango ya Ligi kuu itakwenda sawa kwa kuwa kila kitun nni mpangilio.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad