Akamatwa 'akijiibia gari lake' alipwa fidia nono

Bwana mmoja aliyekamatwa 'akijiibia gari lake' alipwa fidia nono
Bwana mmoja ambaye alitiwa nguvuni na polisi jijini Illinois, Chicago Marekani kwa wizi wa gari ambalo ilibainika kuwa ni mali yake amefikia makubaliano ya nje ya mahakama na mamlaka za jiji kumlipa fidia.

Lawrence Crosby, alikuwa mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu cha Northwestern akiwa miaka 25 wakati tukio hilo lilipotokea mwaka 2015.

Mwanamke mmoja alipiga simu polisi wakati Crosby alipokuwa akirekebisha gari yake na kudhania kuwa nimwizi anayejaribu kuliiba.

Marekani yamtambua kiongozi wa upinzani kama rais wa Venezuela
'Watanzania, hawasubutu kuzungumza' aambiwa rais Magufuli
Mamlaka ya Mji wa Evanston watapigia kura baadae juu ya kiasi gani bwana huyo alipwe lakini wakili wake anasema itakuwa dola milioni 1.25.

Timothy Touhy, ambaye ni wakili wa Dkt Crosby, alitaja kima hicho alipohojiwa na gazeti la Chicago Tribune.

Dkt Crosby, ambaye ni Mmarekani Mweusi ameiambia CBS Chicago kuwa tukio lake litasaidia kuangazia suala la ubaguzi wa rangi nchini humo.

Ruka ujumbe wa Twitter wa @EvanstonNow

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad