Breaking News: Matokeo ya Kidato Cha Nne yatangazwa

Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) leo  wametangaza matokeo ya kidato cha nne mwaka 2018 ambapo ufaulu umeongezeka kwa asilimia 1.29 kutoka asilimia 77.09 mwaka 2017 hadi asilimia 78.38.



Wanafunzi 57 wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Tumaini Lutheran Seminari  ya Malinyi mkoani Morogoro baada ya kubaini shule hiyo kuvujisha mtihani huo.



Mbali na kufuta matokeo hayo, Necta imekifungia kituo hicho cha kufanyia mtihani.

Hayo yameelezwa leo Alhamisi Januari 24, 2019 na Katibu Mkuu mtendaji wa baraza hilo, Dk Charles Msonde wakati akitangaza matokeo ya kidato cha nne mwaka 2018 mkoani Dodoma.



Amesema wameagiza wahusika wote kuchukuliwa hatua wakiwemo polisi waliosimamia.

Dk Msonde ameanza kutangaza matokeo hayo leo saa 5:00 asubuhi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad