Irene Uwoya "Nipo Tayari Hata Kuhudhuria Harusi Ya Dogo Janja"


Muigizaji wa Bongo movie na mrembo anayetrend Hivi sasa kwenye Mitandao ya kijamii Irene Uwoya ameibuka na kusema kuwa hana tatizo na aliyekuwa mume Wake Dogo Janja.

Irene Uwoya na Ex Wake staa wa Bongo fleva Dogo Janja waliweka wazi kuwa wameachana siku chache zilizopita baada ya kuwa kwenye ndoa kwa miezi kadhaa.

Baada ya kuingia kwenye mvutano mkali Wiki iliyopita na hata kurushiana madongo kwenye Mitandao ya kijamii hatimaye Uwoya amesema hana Bifu na Dogo Janja na Hivi sasa ana maisha yake na hata ikitokea amealikwa kwenye engagement party ya Dogo na Mpenzi Wake Mpya ataenda.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ayo, Uwoya ameweka wazi kuwa Ndoa Yake na Dogo Janja imevunjika Lakini sio kitu cha ajabu kwani ndoa nyingi zimeshawahi kuvunjika katika siku za nyuma.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad