Mboso Awaomba Radhi Mashabiki Wake Kisa Hiki Hapa

Mboso Awaomba Radhi Mashabiki Wake Kisa Hiki Hapa
Msanii wa muziki Bongo kutokea lebo ya WCB, Mbosso amewaomba radhi mashabiki wake kufuatia kuchelewa kutoa video ya wimbo wake mpya.

Wimbo huo unaokwenda kwa jina la Tamu ulitoka December 22 mwaka jana lakini video yake rasmi
imekuja kutoka siku ya leo.

"Kwanza naomba radhi kwa kuchelewa kwa Video ya wimbo wenu huu pendwa, Tamu ni changamoto na mitihani ya hapa na pale ambayo ilikuwa nje ya uwezo wangu ilikwamisha kutoka kwa Wakati," ameeleza Mbosso.

Video hiyo imeongozwa na Director Kenny kutoka Zoom Production, hadi sasa wimbo huo umefikisha watazamaji (views) zaidi ya 20,000 ndani ya saa moja  tangu ilipotoka.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad