Nandy Akataa Kufananishwa na Daimond, Alikiba

Nandy Akataa Kufananishwa na Daimond, Alikiba
Msanii wa Bongo Fleva, Nandy amesema si sawa kwa yeye kufananishwa kimafanikio na wasanii wakubwa waliomtangulia kimuziki.

Akizungunza na  Clouds FM amesema yeye bado ana muda mfupi kwenye muziki, hivyo anahitaji kukua zaidi.

"Nina miaka miwili kimuziki na kuna wasanii wapo kwenye game muda mrefu na mimi najivunia uwepo wao kwenye game hivyo sidhani kama ni sawa kufananishwa nao maana hata wao walianza kupokea mkwanja wa show muda kabla," amesema Nandy.

Diamond na Alikiba ni wasanii ambao kwa sasa wanatajwa kuwa na fedha nyingi zaidi kutokana na show za fedha nyingi wanazofanya.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad