Simba Wawashushia Kichapo Cha Mbwa Mwizi Waarabu


Mshambuliaji wa kimataifa wa timu ya Simba anawanyanyua mashabiki wa Simba kwa kuwafanya Simba wapate mabao 3-0 dhidi ya JS Saoura katika Uwanja wa Taifa ukiwa ni mchezo wa kimataifa wa Ligi ya Mabingwa Afrika. 

Dakika ya 45 Okwi alifanikiwa kutumia uwezo wake wa mguu wa kushoto kumalizia pasi ya Clyetous Chama ambaye alipiga pasi mpenyezo iliyomkuta Okwi akawaminya mabeki waarabu na kumalizia kwa shuti kali. 

Dakika ya 52 Okwi anamtengenezea pasi Kagere ambaye anaandika bao la pili kwa Simba. 

Dakika ya 67 Kagere anamalizia pasi ya Okwi na kuandika bao la tatu kwa Simba Uwanja wa Taifa. 

Mbelgiji anafanya mabadiliko ya dakika ya 86 Okwi anatoka anaingia Shiza Kichuya. 

Kwa sasa mpira ni kipindi cha pili huku kila timu ikiwa imepania kupata matokeo, katika harakati za kipindi cha kwanza nahodha John Bocco alipata majeraha akatoka nafasi yake ikachukuliwa na Meddie Kagere. 
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad