Thierry Henry Akalia Kuti Kavu Monaco Muda Wowote Kutimuliwa

Thierry Henry Akalia Kuti Kavu Monaco Muda Wowote Kutimuliwa
Klabu ya soka ya Monaco ipo mbioni kumtimua kazi legendari wa timu ya Arsenal, Thierry Henry kutokana na matokeo mabovu anayoendelea kuyapata.


Henry huwenda akatimuliwa baada ya kuiyongoza klabu hiyo inayoshiriki Ligue 1, tangu mwezi Oktoba.

Mwishoni mwa wiki iliyopita Monaco ilikubali kipigo cha mabao 5 – 1 dhidi ya Strasbourg na kuifanya timu hiyo kushika nafasi ya 19 kwenye msimamo wa ligi.

Vyombo mbalimbali vya habari vimeripoti kuwa Monaco huwenda wakamrudisha aliyekuwa kocha wake, Leonardo Jardim ambaye nafasi yake ilirithiwa na Thierry Henry.


Mshindi huyo wa kombe la dunia mwaka 1998 amejikuta akiingia kwenye majanga tangu kuanza kazi yake ya ukocha kwa mara ya kwanza baada ya kushinda mechi miwili pekee kwenye michezo 12 aliyoiongoza Monaco huku akishindwa kupata hata ushindi mmoja kwenye uwanja wa nyumbani wa Stade Louis II.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad