Tumekoma Hatuwezi Kurudia Tena Makosa-Babu Tale

Tumekoma Hatuwezi Kurudia Tena Makosa-Babu Tale
Meneja wa Kampuni ya Wasafi (WCB) Babu Tale amekiri kuwa adhabu waliyopewa wasanii wake Diamond na Raymond Mwakyusa’ Rayvanny kufungiwa miezi miwili, imewafundisha na hawatarudia tena.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la mwananchi, Babu Tale ameweka wazi kuwa adhabu waliyopata Diamond na Rayvanny imekuwa somo kwao wote na hawatorudia tena makosa.

Kwa kweli kwa muda wote ambao wasanii wetu walikuwa wamefungiwa pamoja na kusitishwa kwa tamasha letu la Wasafi, tumejifunza mengi, hatuna budi kuishukuru BASATA na serikali kwa ujumla tunachowahaidi ni kwamba tumrjifunza mengi na hatutarudia tena”.

Diamond na Rayvanny walifungiwa mwaka jana Desemba 15 na kuzuiwa kufanya maonyesho ya nje na ya ndani hata hivyo Wiki chache zilizopita BASATA Ilitangaza kuwafungulia rasmi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad