Wanawake Wajifua Kung Fuu Kupambana na Wahalifu Mtaani..


Wanawake wanaoishi maeneo ya mabanda nchini Kenya wamejitolea kukabiliana na ukosefu wa usalama katika maeneo yao, jukumu ambalo kwa muda mrefu liliachiwa wanaume.


Wanawake wanaoishi maeneo ya mabanda nchini Kenya wamejitolea kukabiliana na ukosefu wa usalama katika maeneo yao, jukumu ambalo kwa muda mrefu liliachiwa wanaume.


 Kupitia mpango walioupa jina ‘wamama na usalama' wanawake hao wanasema wanatambua jukumu lao kubwa la kuielekeza jamii ndiposa wanataka kuwa mstari wa mbele katika harakati za kukabiliana na ukosefu wa usalama. 


Maeneo ya mabanda yanasifika kwa kila aina ya uhalifu hali inayochangiwa na wingi wa watu, umasikini na kiwango kikubwa cha ukosefu wa ajira.


 Kina mama na watoto huathirika zaidi kutokana na visa vya uhalifu katika maeneo hayo huku vijana wakilaumiwa zaidi kwa kusababisha uhalifu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad