Baada ya kuachana na Irene Uwoya, Dogo Janja amtambulisha Mpenzi Wake Mpya

Baada ya kuachana na Irene Uwoya, Dogo Janja amtambulisha Mpenzi Wake Mpya
Msanii wa muziki wa Bongo fleva Abdul Chande maarufu kama Dogo Janja ameibuka na kumuweka hadharani Mpenzi wake  Mpya anayejulikana kwa jina la Linah.

Dogo Janja aliachana na aliyekuwa mke Wake Msanii Irene Uwoya mapema mwaka jana Baada ya kukaa kwenye ndoa kwa miezi kadhaa.

Baada ya ndoa hiyo kuvunjika wasanii hao walikataa kuliweka wazi suala hili hadi pale Irene Uwoya alipoonekana anakula bata nje ya nchini akiwa mwenyewe bila Dogo Janja

Siku ya jana Dogo Janja amemtambulisha mpenzi wake huyo mpya kupitia ukurasa wake wa Instagram ikiwa ni siku ya mpenzi wake huyo ya kuzaliwa.

Dogo Janja aliandika maneno haya:-
“Hakuna neno linaloweza kutosha katika kuielezea furaha niliyonayo kwenye kufurahia siku yako ya kuzaliwa mpenzi wangu..mengine nitakuelezea chumbani.. Kula ushibe, Kisha kaza chaga… nakupenda sana❤️❤️❤️❤️ @quenlinnatotoo #BuddahBossPonDiLove“

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad