Baada ya Kuandamwa Mitandaoni Kisa Kauli Yake kwa Ommy Dimpozi, Steve Nyerere Aibuka na Kupangua Tuhuma " Sikusema Hivyo Watu Wameninukuu Vibaya"

Baada ya Kuandamwa Mitandaoni Kisa Kauli Yake kwa Ommy Dimpozi, Steve Nyerere Aibuka na Kupangua Tuhuma " Sikusema Hivyo Watu Wameninukuu Vibaya"
Msanii wa Bongo movie ambaye ni maarufu kwa kuiga sauti za viongozi mbali mbali w serikali, Steve Nyerere amefunguka na kuongelea skendo inayomuandama hivi sasa dhidi ya Msanii wa Bongo movie Ommy Dimpoz.

Siku za nyuma kidogo Steve Nyerere alifanya mahojiano na kituo kimoja cha habari na kusema Ommy Dimpoz hawezi kuimba tena kwa sababu ya hali ya ugonjwa wake, huku akiwaomba Watanzania kumuombea na kuwa naye karibu ili apate faraja na kupona.


Baada ya sakata hilo Steve Nyerere ameibuka na kusema maneno hayo yanayosambazwa hayana ukweli kwani yeye hakusema hataweza kuimba kabisa bali alisema hataweza kuimba kwa wakati ule.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ayo, Steve Nyerere amefunguka haya:

Kwanza niseme kuwa yupo kwenye dunia ya kubadilisha maneno na ya kugombanisha watu, Mimi sipo huko…Unapomzungumzia Steve Nyerere unakuwa unazungumzia brand , mzigo mkubwa sana usikaone hivi”.

Siachagi kunukuu kitu nilichokisema, nilisema hatoweza kuimba tena kwa muda huu, Aki-recover sijui mnaelewa maana ya ku-recover”.

Ommy Dimpoz ameweka wazi kuwa ameshangazwa na kauli ya Steve Nyerere kuwa kutokana na ugonjwa Wake hatoweza kuimba hasa ukizingatia Steve hajawahi kumtafuta kumjulia hali kipindi chote alivyokuwa mgonjwa

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad