Dudu Baya Mikononi mwa Polisi Kisa Ruge

Dudu Baya Mikononi mwa Polisi Kisa Ruge
Msanii wa muziki Bongo, Dudu Baya leo anatarajiwa kufika kituo cha Polisi Posta Dar es
Salaam mara baada ya kupigiwa simu na polisi na kutakiwa kufanya hivyo.

Utakumbuka mapema jana Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Harrison
Mwakyembe aliliagiza Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa kushirikiana na Polisi kuhakikisha
wanamkamata Msanii DUDU BAYA kwa kosa la kukashifu na kutoa lugha za kejeli kwa Marehemu
Ruge Mutahaba.

Hatua hiyo ilifikiwa mara baada ya Dudu Baya kutumia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram kutoa lugha isiyofaa kimaadili kwa Marehemu Ruge.

Ruge Mutahaba ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group (CMG)amefariki siku ya jana nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu ya figo. Ruge alizaliwa mwaka 1970, Brooklyn nchini Marekani, atakumbukwa zaidi kwa mchango wake mkubwa katika sekta ya muziki nchini.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad