Faiza Asifiwa Kapendeza Baada Ya Kuacha Kuvaa Nusu Utupu

Msanii wa Bongo movie na mzazi mwenzake na Mbunge wa Mbeya Mjini Sugu, Faiza Ally amesifiwa kupendeza na mavazi ya heshima baada ya kuachana na mavazi ya nusu uchi.

Mashabiki waliomuona kwenye moja ya Shughuli Hivi karibuni wamesema kwamba amebadilika katika suala zima la mavazi tofauti na zamani ambapo alikuwa akijiachia nusu utupu akiwa kwenye matamasha.


Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Faiza amefunguka na kusema kuwa aliamua kuvaa vazi la heshima kwani hakutaka kuongelewa sana kwani amekuwa mtu wa kuongelewa kwenye kila red carpet event.

Faiza ameshawahi kuzua gumzo siku za nyuma Baada ya kuvaa nguo iliyokuwa inaacha makalio yake wazi kutokana na kuchanwa chanwa Lakini pia Faiza ameshawahi kuvaa shati la kiume tu na tai.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad