Hatimaye Uwoya Azindua Bar Yake Aja na Muonekano wa Kipekee

Hatimaye Uwoya Azindua Bar Yake Aja na Muonekano wa Kipekee
HII ni noma! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya staa wa filamu za Kibongo, Irene Uwoya kufanya kufuru ya aina yake na kuwakalisha mastaa wenzake, Wema Sepetu na Aunt Ezekiel.



UWOYA ameonekana kuwakalisha Wema na Aunt baada ya kuteketeza mamilioni ya fedha katika matengenezo ya baa yake inayojulikana kwa jina la New Last Minute Lounge iliyopo Sinza jijini Dar ambayo matengenezo yake yamechukua muda mfupi.

Uwoya amezindua baa Yake Ambayo imeonekana kuwa na ubunifu wa aina yake kwa kupamba na picha za mastaa ambao sasa ni Marehemu


Wema na Aunt wamekalishwa na Uwoya kwani biashara zao wanazozifanya haziwezi kufikia hatua aliyonayo Uwoya kwani Wema anamiliki duka la nguo za watoto huku Aunt akimiliki baa ambayo siyo ya hadhi hiyo. Baa hiyo ya Uwoya inatarajiwa kuzinduliwa rasmi kesho ambapo watu mbalimbali pamoja na mastaa watakuwepo kushuhudia ilivyo ya hadhi ya kistaa.

Amani lilifanikiwa kufika kwenye baa hiyo yenye eneo kubwa na kujionea vitu vingi vya thamani na vya kisasa huku ulinzi wa eneo hilo ukiwa umeimarishwa kwani haruhusiwi mtu yeyote kukatiza ama kuingia eneo hilo kama hana kitu cha muhimu cha kufanya. Miongoni mwa vitu vya thamani vilivyomo ndani ni pamoja na viti, meza na masofa ya kisasa, jiko zuri la kupikia na kuchomea nyama, sehemu nzuri ya vinywaji na vingine vingi.

Ndani ya baa hiyo pamoja na kuwa na vitu vya thamani pia kuna vinavyoshangaza kwani ukutani kumepambwa na picha za mastaa mbalimbali ambao wameshafariki dunia akiwemo aliyekuwa rafiki yake kipenzi, marehemu Agnes Gerald ‘Masogange’, Rachel Haule, Bi Kidude, Steven Kanumba, Albert Mangwea ‘Ngwea’, Amri Athuman ‘Mzee Majuto’, Adam Kuambiana, Langa Kileo, Sharo Millionea na wengine wengi.

Mbali na picha hizo pia kuna sehemu tatu nzuri na zenye utulivu kwa ajili ya kunywea vinywaji na vyakula, ambapo mteja akikaa hawezi kuboreka kwani kuna hali ya hewa nzuri, TV kubwa yenye inchi 42. Baada ya Amani kutalii ndani ya baa hiyo, waandishi wetu waliweza kuzungumza mawili matatu na walinzi kuhusiana na uzinduzi utakavyokuwa;


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad