Jakaya Kikwete: “Nimelemewa, Huzuni, Majonzi, Taifa Limepoteza Mtu Mahiri”

Raisi Mstaafu wa awamu ya nne Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amefunguka kuguswa na msiba wa aliyekuwa Mkurugenzi wa vipindi Clouds Media Group Ruge Mutahaba.

Raisi Kikwete Kupitia ukurasa wake wa Twitter amefunguka hudhuni yake Baada ya kufariki Ruge na kuweka wazi kuwa katika kipindi kigumu cha maombolezo:


Nimelemewa! Nakosa maneno ya kuelezea huzuni na majonzi niliyonayo kwa kifo cha Ruge Mutahaba. Taifa limepoteza kijana wake mahiri, mbunifu na mzalendo wa kweli. Nimepoteza rafiki, mshirika mwaminifu na mtu ambaye amenisaidia kwa mengi ktk uongozi wangu na hata baada ya kustaafu”

“Moyo wangu uko pamoja na wazazi wake, ndugu zake na familia yake katika kipindi hiki kigumu. namuombea kwa mola ampe mapumziko mema peponi. Ameen.”



Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad