Lema Afunguka Walivyomtorosha Zitto Kabwe

Mbunge wa Arusha Mjini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Godbless Lema amesema kuwa  Jumatano Februari 6, 2019 walilazimika kumuondoa mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe baada ya kufuatiliwa na watu ambao hakuwataja.

Ameyasema hayo jana wakati akichangia taarifa ya Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ambapo amesema kuwa kama Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikitawala kwa haki, kwa kufuata sheria na Katiba hana tatizo hata kikitawala milele.

“Leo mwenyekiti (Mussa Azzan Zungu), Zitto hayuko bungeni tumemuondoa juzi alikuwa anafuatiliwa usiku kwa kazi za kibunge, sio za kuuza madawa ya kulevya si za kubaka watoto ni kazi za kibunge.”alisema Lema

Lema aliongeza kwa kusema kuwa lengo lao ni kuona wanatawaliwa na CCM  kwa haki na ndio maana ya upinzani lakini leo hii chuki inajengwa na baadhi ya viongozi ambao wamekuwa wakitoa kauli tata dhidi ya upinzani

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad