Lulu Afungukia Tetesi Za Kuwa na Mimba

Lulu Afungukia Tetesi Za Kuwa na Mimba
Msanii wa Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu amefunguka na kuweka wazi kuwa sio mjamzito na hata alipotoka gerezani hakuwa mjamzito.

Lulu alitoka gerezani mwaka jana Baada ya kutumikia kifungo kwa miezi kadhaa lakini Baada ya kutoka kuna tetesi zilisambaa kuwa ametoka mapema kutokana na ujauzito na pia alikuwa ameongezeka kwa kiasi kikubwa.


Lakini siku ya Leo kwenye mahojiano aliyofanya na Times Fm, Lulu ameweka wazi kuwa hajawahi kuwa mjmzito kabisa bali alinenepa alipokuwa jela na kuongezeka karibia kilo 20.

Lulu amesema taarifa zilizowahi kusambaa kuwa alikuwa mjamzito hazily was za kweli bali alivyotoka jela alikuwa ameongezeka kilo 20 hivyo kupelekea mwili Wake kuwa mkubwa sana.

Lakini pia amefungukia tetesi za kugombana na Mpenzi Wake Majizzo ambapo amesema kuwa hawezi kuongea chochote kuhusu maisha yake binafsi:

Watu wanatengeneza vitu vyao ili wapate jambo kutoka kwako, watu wanatengeneza mambo yao, Mimi kuwa maarufu haimaanishi kila kitu katika miasha yangu lazima kiwe maarufu, hata mahusiano yangu yawe maarufu.

Juu ya hilo la kuvua pete Siwezi kukubali wala kukataa wacha waamini wanavyoamini”.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad