Mange Kimambi Amshukia Diamond Platnumz...Amtaka Amsamehe Baba yake ili Apate Amani

From @mangekimambi_ - Hii posti nilitaka kuposti since last week. Niliiacha kwenye drafts. Naona iki subiri 1 month ita expire 🤣

Diamond pls msamehe babako. Wenzenu tunalia kila siku kuwakosa wazazi wetu nyinyi wenzetu wenu wako hai alafu hamuwataki??😭😭😭 Msamehe huyu mzee, msamehe mara 70. Wewe mwenyewe huwezi kuwa sawa deep down kutokuelewana na huyu mzee. Hakuna binadamu anaweza kuishi a peaceful happy life bila kuelewana na mzazi wake aliemleta duniani. Uta pretend to be happy but deep down you will never be, something is missing. Inawezana huwezi ku connect dots ila hii situation na baba yako inachangia sana wewe kushindwa kuwa baba kwa watoto wako uliowazaa. Wengi hawawezi kukwambia ila let me tell you this ni mwanaume mwenye matatizo pekee anaweza kukaa karibia mwaka mzima hamjamtia mtoto wake machoni wala hajui mwanae anakula nini au anaishi vipi na anakaa nae hapo hapo Dar. Na mzizi mkubwa ni mahusiano yako na baba yako. Na wewe unawafanyia watoto wako kile kile alichokufanyia baba yako. It’s almost like unawalipizia watoto wako alichokufanyia baba yako. Kuna interview ulisemaga baba yako alikuwa na uwezo sana tu enzi hizo na hakukusaidia, hili ni fundisho kubwa kwako hata wewe 20 years from now unaweza kuwa huna kitu na watoto wako ndo wakazishika na wao watakukazia kama wewe unavyomkazia mzee wako na mama zao ndo watawatia sumu mpaka . Tafadhali Diamond break the circle. Acha hii kitu iishie kwako isiendelee kwa kizazi chako pia.

Pia niamini napokwambia kuwa siku dingi ako akifa na hujaelewana nae utatamani ukamchimbue kaburini umwambie umemsamehe..... Utatamani urudishe nyuma muda uelewane nae. Siku huyu mzee akifa hakuna mtu atakae umia zaidi yako wewe sababu ya guilt, na utaumia zaidi vile hutoweza kuexpress uchungu yako msibani sababu kila mtu atakushangaa why unamlilia na huku alipokuwa hai hukutaka hata kupokea simu yake? Hakuna kifo kitakachosumbua nafsi yako kama cha huyu mzee iwapo utaruhusu aingie kaburini kabla hujaelewana nae....

You are a not bad person, naamini huyu mzee amekuumiza mno but this is your father. Lazma umsamehe ili hata wewe mwenyewe upate amani ya kweli. Utapata thawabu kubwa ukiweza kumsamehe baba yako na kusahau yaliyopita.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mange yuko sahihi kibinadamu, lakini msamaha halisi ni ule utakaotoka moyoni, siyo ule unaokuja kwa vile ama "nimeombwa na mashabiki wangu" au kwa vile "nimekuonyesha utemi wangu hadi ukanilamba miguu yangu na kila mtu anajua sasa baina yangu na wewe ni nani zaidi." Baraka Obama alimtafuta sana baba yake aliyemwacha akiwa na mwaka mmoja akalelewa na baba wa kufikia na hakuweza kumwona baba yake mzazi tena. Hata hivyo bado hadi leo anajua mchango wa damu ya baba yake katika uhai wake na ndiyo maana anamheshimu sana mama mzazi wa baba yake pamoja na ndugu zake wengine wa kwenye line ya baba yake. Mungu ana mitego mingi sana duniani hapa kwa wajane wake; mmoja wapo unaweza kuwa ni huu.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad