Mshahara wa Tundu Lissu Kusimamishwa Kisa Hiki Apa Spika Anena

Mshahara wa Tundu Lissu Kusimamishwa
Spika wa Bunge, Job Ndugai (Mb) amesema kuna haja ya kusimamisha mshahara wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kwa sababu hayupo bungeni, jimboni kwake wala hospitalini, na hajapewa taarifa zozote na daktari.

Spika Ndugai ametoa taarifa hiyo Bungeni wakati akijibu Muongozo wa Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Msukuma ambapo amesema Mbunge huyo hayupo Hosipitali,Hayupo Bungeni na hayupo Tanzania wala hajulikani anafanya kitu gani huko aliko hivyo hana sababu ya kuendelea kulipwa.

Tundu Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, yupo katika ziara ya siku 10 nchini Marekani baada ya kufanya hivyo kwenye nchi za Ujerumani na Uingereza.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad