Mwalimu Mkuu Jela Miaka 6 Kwa Kuiba Fedha za Shule

Mwalimu Mkuu Jela Miaka 6 Kwa Kuiba Fedha za Shule
Mwalimu  Mkuu  shule ya  sekondari  Mikwambe, Paulo Lorry, amehukumiwa kifungo cha miaka sita na kutakiwa kulipa Sh milioni 16 katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke alizoiba kutoka akaunti ya shule.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na  Mkuu wa Taasisiya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa wa Temeke, Pilly  Mwakasege, ilieleza kuwa mwamu Lorry amekutwa na hatia na kuhukukiwa kwenda jela.

Ilieleza kuwa mwalimu huyo alishtakiwa na makosa matatu ya matumizi  mabaya  ya  ofisi  kifungu   cha  31  cha   Sheria ya  Kuzuia na Kupambana na  Rushwa  namba  11/2007  kama ilivyofanyiwa  marekebisho  mwaka  2002.

Mshitakiwa  alikuwa  ni  Mwalimu  Mkuu wa  Shule  ya  Sekondari  Mikwambe  Manispaa ya  Temeke    mwaka  2010  alipokea Sh milioni 28 kupitia  akaunti  ya  shule  namba  CA 2011100236 kwa  ajili  ya  ujenzi wa  maabara  shuleni  hapo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad