Mwanaume Aua Kwa Kumkapa Koo

Mwanaume Aua  Kwa Kumkapa Koo
Bwana mmoja nchini Marekani amemuua Simba wa milimani ambaye alimshambulia ghafla mbugani.

Simba huyo dume alimvamia kwa nyuma bwana huyo ambaye hakutajwa jina lake katika Hifadhi ya Wanyama ya Colorado.

Maafisa wanyamapori wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo siku ya Jumatatu ambapo mwanaume huyo amepata majeraha makubwa usoni na kwenye kiganja cha mkono.


Bwana huyo alikuwa akifanya mazoezi kwenye ukanda maalum kwenye mbuga hiyo ambao hupendelewa kutumiwa na wakimbiaji wakati tukio hilo lilipomkuta.

Maafisa wanasema aligeuka nyuma baada ya kusikia mnurumo nyuma yake nap apo hapo simba huyo akamrukia usoni.

"Simba alimrukia mkimbiaji huyo, na kumng'ata usoni na kiganjani. Lakini alifanikiwa kujinasua kutoka kwenye makucha yake na kisha kumuua," taarifa rasmi ya hifadhi hiyo imeeleza.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad