“Nakupenda Sana, Kula Ushibe Halafu Kaza Chaga”-Dogo Janja


Msanii wa muziki wa Bongo fleva Abdul Chande maarufu kama Dogo Janja ameibuka na kumtumia ujumbe Mpenzi wake  Mpya anayejulikana kwa jina la Linah.

Dogo Janja alitangaza kuchana na aliyekuwa mke Wake Msanii Irene Uwoya mapema mwaka jana Baada ya kukaa kwenye ndoa kwa miezi kadhaa.

Dogo Janja Hivi sasa yupo kwenye mahusiano na Mrembo ambaye ni Mfanyabiashara kutoka Arusha ambaye anasemekana kuwa na pesa ndefu kutokana na Familia yake kuwa kwenye biashara za madini.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Dogo Janja amemtumia ujumbe wa birthday mrembo huyo ambaye alizaliwa siku ya jana:

Hakuna neno linaloweza kutosha kuielezea furaha niliyonayo kwenye kufurahia siku yako ya kuzaliwa mpenzi wangu…..mengine nitakueleza chumbani…..kula ushibe kisha kaza chaga….nakupenda sana”.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad