Rapa Country Boy Amuanika Mpenzi Wake

Rapa Country Boy Amuanika Mpenzi Wake
Msanii wa muziki wa hip hop nchini Country Boy amefunguka na kuweka wazi hali ya mahusiano ya kimapenzi na mwanamke aliyekuwa naye kwa Hivi sasa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha XXL cha Clouds Media, Country Boy ameongelea Hadharani mapenzi yake kwa mara ya kwanza ambapo amesema:


Nipo kwenye mahusiano na najua watu wengi hawakunizoea kuniona nikiweka wazi mahusiano yangu, Mtu ambaye nipo nae alikuja kwenye maisha yangu kipindi ambacho sikuwa sawa lakini alionyesha upendo na ana nafasi kubwa sana kwangu kwani ni mshauri mzuri na anapenda ninachokifanya na hata muda huu ananisikiliza ili kuhakikisha kama kweli nimefika hapa kwenye XXL”.

Lakini pia Country Boy pia amefungukia uhusiano Wake na msanii mwenzake anayeitwa Young Lunya ambapo alisema:

Mimi na Young Lunya ni washkaji wa kitambo na nakumbuka tulikutana mwaka 2012 kwenye kumbi ya starehe na yeye alikuwa amepoteza buku na sisi ndiyo tuliyoiokota na kuanzia hapo ukaribu ukaanza, Tunakuja na ngoma yetu mimi Babuu pamoja na Lunya”.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad