'Rose Mhando Anahitaji Maombi na Wala Sio Maneno Maneno' Sayuni Mrita.


Sayuni Mrita muimbaji wa injili anayetamba sasa na Wimbo wa YESU AMEFANYA alipoulizwa kuhusu Rose Muhando ambaye ametajwa kukumbana na changamoto nyingi na watu kila mtu kusema lake, Sayuni amejibu

Muimbaji huyo anasema kuwa kinachotakiwa kwa sasa ni maombezi ya nguvu na yenye kumakinika sana kwa Rose Muhando na kuacha kufanya muzaha wa kumsema vibaya msanii huyo.
“Kwa upande wa dada yetu Rose Mhando, ndani yake Mungu alimuwekea hazina kubwa sana. Adui                nae alipopata mlango tu akaingia ili kuiharibu. Kwa bahati mbaya hakuna mtu aliyeweza                              kusimama kikamilifu katika nafasi kumsaidia.

Hivyo ni vyema tukaendelea kumuombea na kumsaidia kuliko kum-discuss na kumsema. Watu                  wengi hawajui shetani yuko kazini wakati wote, na ukishampa nafasi anakutawala na bila kupata                  msaada haraka waweza angamia kabisa”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad