Simba yapata kocha msaidizi

Simba yapata kocha msaidizi
Hivi karibuni mwekezaji na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya klabu ya Simba Mohammed Dewji aliweka wazi kuwa tayari wameshatoa maelekezo kwa CEO wa Simba Crescentius Magori kuhakikisha timu inapata kocha msaidizi jambo ambalo limekamilika.

Nafasi hiyo iliyoachwa wazi mwanzo mwa msimu huu na aliyekuwa kocha msaidizi wa Simba Masoud Djuma, imezibwa na kocha mtanzania Denis Kitambi.

Kitambi amewahi kuzifundisha vilabu vya Ndanda FC akiwa kama kocha mkuu, Azam FC akiwa kocha msaidizi chini ya Stewart Hall ambaye pia alikwenda kufanya naye kazi kama kocha wake msaidizi katika klabu ya AFC Leopards ya Kenya.

Imeelezwa kuwa tayari amekwishajiunga na kambi ya timu hiyo jijini Dar es Salaam ambapo mchezo wake wa kwanza kukaa kwenye benchi la ufundi utakuwa ni dhidi ya Yanga Jumamosi hii.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad