Siwezi Kuitangaza Ndoa Kwenye Mitandao- Lulu


Muigizaji wa Bongo movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu amefunguka na kusema kuwa haweiz akaianika ndoa yake au mipango ya ndoa yake hadharani.

Lulu alivalishwa pete na mchumba wake Mkurugenzi wa EFM Majizzo mwaka jana mwishoni Baada ya kutoka gerezani, Lakini badala ya kusikika mipango ya ndoa kumekuwa kunasikika Tetesi za kuachana.

Skendo kubwa ambayo ilisambaa kwenye Mitandao ya kijamii ni kuwa Majizzo alimpa kipigo Lulu na kupelekea mrembo huyo kuvua pete yake na hata tetesi zinadai ndoa hiyo haipo tena.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Lulu amesema wazi kuwa ndoa ipo Lakini hawezi akaanza kuitangaza kwani ni mambo ya binafsi.

Lulu amesema anataka mashabiki wamsapoti kwenye kazi zake kama ni filamu wanunue na vitu vingine Lakini kuhusu harusi yake haina umuhimu wa kufuatilia kwani hawezi kuwaangalia.

Lakini pia Lulu ameweka wazi kuwa ndoa yake na Majizzo Iko pale pale na maandalizi yanaendelea .

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad