TRA Yafafanua mabango kwenye magari kudaiwa kodi

TRA Yafafanua mabango kwenye magari kudaiwa kodi
Baada ya kusambaa kwa barua ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ikimtaka mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya International Tanfeed Limited kulipia Sh1.8 milioni za kodi ya tangazo katika gari la kampuni hiyo, mamlaka hiyo imefafanua juu ya kodi hiyo.

“Kuna mabango ya kawaida yamesimikwa, mabango yaliyo juu ya majengo na mabango ya kwenye magari ambayo gari kila likizunguka linakuwa na bango hilo, mfano kampuni za vinywaji, biashara ya bidhaa mbalimbali,” alisema mkurugenzi wa elimu kwa mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo.

“Sio kodi mpya na si kitu cha ajabu, magari haya yanastahili kulipiwa. Kwa mfano, bango lipo katika gari linazunguka nchi nzima linaonwa na watu wengi zaidi kuliko bango likiwekwa sehemu moja.”

Alisema matangazo yote yakiwamo yaliyo kwenye magari mbalimbali yanatakiwa kulipiwa ada ya mwaka kwa mujibu wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2017.

Katika barua hiyo ya Novemba 26, mwaka jana, meneja wa TRA mkoa wa kikodi wa Kinondoni alimtaka mkurugenzi wa kampuni hiyo kulipa kodi ya Sh1.8 milioni kwa matangazo yaliyomo katika gari hilo kwa mujibu wa sheria kupitia mfumo wa ukusanyaji mapato wa TRA kupitia namba GFS Code 14220177.

“Zingatia kwamba ikitokea umeshindwa kulipa kama ilivyobainishwa hapa (kwenye barua), mamlaka itatafuta namna ya fidia kiasi hicho dhidi yako kama ilivyobainishwa katika Sheria ya Kodi,” inasomeka sehemu ya barua hiyo.

Awali, kodi za matangazo ya mabango zilikuwa zikikusanywa na Serikali za Mitaa lakini baada ya kupitishwa kwa Sheria ya Fedha ya mwaka 2017, kodi hizo sasa zinakusanywa na TRA.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad