Trump adaiwa kuchochea 21 Savage aondolewe Marekani


Kupitia mahojiano aliyoyafanya 21 Savage na kipindi cha televisheni cha Good Mornig America ameelezea kuwa kukamatwa kwake ulikua kama mtego kutokana na Maafisa wa Uhamiaji kumkamata kwa nguvu bila kutoa sababu yoyote zaidi ya kuwasikia wakisema ‘tumempata 21 Savage”.

Ikiwa tayari ni siku 10 zimepita tangu Rapper 21 Savage akamatwe na idara ya Uhamiaji nchini Marekani amefunguka kuhusiana na sakata hilo ambapo February 14,2019 21 Savage aliachiwa kwa dhamana na kuripotiwa kuwa Rais wa Marekani Donald Trump anachochea ishu ya 21 Savage kurudishwa Uingereza.

“Sijui nini kilitokea zaidi ya kuona bunduki na taa za blue nilipokuwa naendesha gari na hawakusema chochote zaidi ya kusema tumempata Savage nina uhakika ilikua ni mtego au lengo lao” >>> 21 Savage

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad