Tume ya Uchaguzi Nigeria yakanusha kushawishiwa kisiasa


Huku wagombea uchaguzi nchini Nigeria wakishutumiana kwa tangazo la ghafla la kuahirishwa uchaguzi, tume ya uchaguzi inasema kuwa tangazo hilo halikushinikizwa kisiasa wala kiusalama.

Uamuzi huo uliotangazwa masaa matano tu kabla ya vituo vya kura kufunguliwa siku ya Jumamosi unatajwa kuigharimu nchi hiyo dola bilioni 2 za Kimarekani, sambamba na kuiathiri hadhi ya taifa hilo kubwa kabisa kufuata mfumo wa kidemokrasia barani Afrika.

Kwa sasa, mamlaka zinazohusika na uchaguzi zina kazi ya kuamua namna ya kuvifanya vifaa vya kupigia kura ambavyo tayari vilishawasilishwa kwenye vituo vya kupigia kura, huku hali ikiwa ya wasiwasi kutokana na matukio ya hivi karibuni ambapo majengo ya tume ya uchaguzi yalichomwa moto.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi, Mahmood Yakub, aliwaambia waangalizi, wanadiplomasia na waandishi wa habari kwamba kucheleweshwa huku kwa uchaguzi hakuhusiani na hali ya ukosefu wa usalama wala kuingiliwa kati kisiasa. Badala yake, mwenyekiti huyo alisema "mazingira mabara" ikiwemo hali mbaya ya hewa ndiyo iliyopekelea kuchelewa kwa ndege zilizobeba vifaa na pia moto kwenye ofisi tatu za tume yake.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad