Waziri Mwakyembe apiga 'STOP' kuita uwanja wa Taifa kwa Mchina


Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amepiga marufuku uwanja wa Taifa kuitwa kwa Mchina huku akiomba uwanja huo usiitwe hivyo.

Mwakyembe ameyasema hayo leo kwenye mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kuzindua rasmi nembo itayotumika kama ishara za fainali za michuano mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 (AFCON-U17).

Katika uzinduzi huo alitumia fursa  kuwaonya watu na wadau wa soka ambao hawajivunii kuwa na uwanja wa Taifa kwa kuliita jina hilo.

"Hebu tuwe waangalifu kidogo kwenye kuanzisha misemo na vibwagizo kwenye michezo ambavyo vinaweza kupotosha na visisaidie sana kujenga utaifa, kwa mfano imejitokeza fashion sasa ya kuita uwanja wa Taifa kwa Mchina, mimi naomba tu niseme wazi huu ni upuuzi uliopitiliza, naomba msiite uwanja huu kwa mchina, uwanja huu hatukupewa zawadi na mchina ulitokana na kodi ya Mtanzania," Dkt. Mwakyembe

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad