Wema na Diamond Uso Kwa Uso Waishia Kukumbatiana


Msanii wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz amekutana uso kwa uso na aliyekuwa Mpenzi Wake Wema Sepetu katika mkutano siku ya jana.

Diamond alikutana na Wema uso kwa uso katika mkutano uliofanywa na mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda wakati anaongea na wasanii Mbali Mbali.

Diamond alionekana akisalimiana na Wema kwa Kumkumbatia kamaalivyo wakumbatia wasanii wengine mbali mbali waliokuwa katika ukumbi huo.

Kama utakumbuka mara ya mwisho Wema na Diamond walipoonekana wanakumbatiana mbele ya hadhara Zari alithibitisha kuwa Wema bado alikuwa anatembea na Mondi na hata kumtuhumu kwa kuvunja mahusiano yake na Diamond.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad