Wolper Alizwa na Vifo Vya Watoto Njombe

Wolper Alizwa na Vifo Vya Watoto Njombe
Mastaa mbali mbali wamejitokeza kukemea vitendo vya mauaji dhidi ya Watoto ambayo yanaendelea mkoani Njombe Hivi sasa.

Kwa Wiki karibuni chache sasa kumekuwa na mauaji makubwa ambayo yanafanyika katika vijiji vya mkoa wa Njombe ambapo Watoto wamekuwa wakiuliwa kikatili kwa kuchinjwa.


Msanii wa Bongo movie Jacqueline Wolper amekuwa mstari wa mbele kukemea vitendo hivyo ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika maneno haya:

Jesus eti Nini kina endelea sijaelewa 😳 Hii ni Tanzania Then why 🙆‍♀️How🤔 Coment This kwa wanaojua Na poleni Wote“.

Lakini pia Haji Manara amekemea pia kitendo gaucho ambapo ameandika:

Tupaze sauti zetu wote kukemea dhulma hii!! Watoto wanayo haki ya kuishi,haki ya kusoma na wanayo haki ya kucheza na kufurahi! Why wauawawe ? Ndugu zangu hili ni jukumu letu sote kuwalinda watoto wetu,kulilinda Taifa letu la baadae,tusikubali udhalimu huu,na tuseme NO!! Inaumiza sana kuona yupo Mtanzania anafanya ukatili huu kisa ni imani potofu za kishirikina!!
Khofu ya Mungu ipo wapi? Ohhh Watoto wetu nn kosa lao? Au kuzaliwa watanzania? ! Mwenyezi Mungu kwako tunakukabidhi wauaji hawa waliolaanika.”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad