Anusurika Kufa Baada ya Kukatwa Sehemu Zake za Siri

Anusurika Kufa Baada ya Kukatwa Sehemu Zake za Siri
Mtu mmoja mkazi wa Marangu mkoani Kilimanjaro amenusirika kufa baada ya vijana kumkamata na kuzikatia chini sehemu zake za siri.

Mtu huyo mwenye umri wa miaka 53 amesema, tukio hilo lilimtokea juzi wakati akitoka katika shughuli zake za kila siku ndipo alikutana na vijana wawili ambao walianza kumpiga.

"Nilitoka kazini muda wa saa tatu usiku nikiwa napandisha nyumbani,  nikakutana na vijana, mmoja akanipiga na chuma mgongoni nikaanguka chini, mwingine akachomoa sime akachana suruali nliyokuwa nimevaa na kunikata sehemu zangu,"alisema.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro, Hamisi Issah alisema, tukio hilo lilitokea katika Kijiji cha Marera lole Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani hapa.

Alisema kuwa, mtu huyo alijeruhiwa na kitu chenye ncha kali kwa kukatwa sehemu za siri akiwa maeneo ya karibu na nyumbani kwake.

Alisema kuwa , waliomjeruhi ni Inocent Rubi mwenye umri wa miaka 18 na mwingine anayeitwa Gift Olmekei ambaye ni mtoto wa kike ambaye ni mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kiri na kusema wote wameshikiliwa na Jeshi la Polisi huku uchunguzi ukiendelea kufanyika.

Aliendelea kusema kuwa, mara baada upelelezi utakapokamilika shauri hilo litapelekwa mahakamani ili sheria iweze kuchukua mkondo wake ili waweze kujua mtu huyo alitoka wapi na watoto wadogo ambao ni wanafunzi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad