China Yasitisha Matumizi ya Ndege za Boeing 737 MAX 8 Kisa Hiki Hapa

China yasitisha matumizi ya ndege za Boeing 737 MAX 8, ni baada ya ajali ya Ethiopian Airlines
China imeagiza kampuni zote za ndege nchini humo kusitisha safari za ndege aina ya Boeing 737 Max 8 baada ya ajali ya ndege ya Ethiopia ambayo ni ya muundo sawa na hizo.


Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC, Kampuni za ndege ni lazima zisitishe usafiri wa abiria wa ndege zote za Boeing 737 Max 8 kufikia saa 18:00 kwa saa za huko. Ilisema taarifa kutoka halmashauri ya usafiri wa ndege ya China.

Ajali ya Ethiopian Airlines ni ya pili ya ndege aina hiyo chapa 737 Max 8 katika muda wa miezi mitano iliyopita.Boeing 737 Max-8 ni ndege ya aina gani?

Ethiopian Airlines: Uraia wa abiria waliokufa watambuliwa

Taarifa kutoka halmashauri ya usafiri wa ndege China, imesema, huduma za ndege hiyo zitarejelewa baada ya ”kuthibitisha hatua za kiusalama zimeimarishwa”

Mamlaka hiyo pia imesema itashauriana na halmashauri ya safari za ndege nchini Marekani na wasimamizi wa Boeing.

Taarifa hiyo pia ilisema kuwa raia wanane wa China walikuwa wameabiri ndege iliyohusika katika ajali ya siku ya Jumapili ikiwa safarini kutoka Ethiopian kuenda Kenya iliyoanguka muda mfupi baada ya kupaa kutoka mjini Addis baba.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad