Hamisa Mobetto Ayakimbia Mapenzi

amisa Mobetto ayakimbia mapenzi
Mwanamitindo na Msanii wa Bongo Fleva, Hamisa Mobetto ameonyesha kuwa kwa sasa hayupo tena kwenye mahusiano ya kimapenzi.

Hiyo ni kwa mujibu wa ujumbe aliochapisha kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Instagram hii leo, mrembo huyo ameandika;

"Yani jamani kichwa kinaniuma, jana tu nilikua kwenye relationship leo nipo single. Nahisi kama nimepigwa na radi hivi, sasa jamani jezi za kesho (leo) za kwenda kuangalia Taifa Stars navaa na nani,  na vile vitenge nilivyoshona Sare," ameeleza Hamisa Mobetto.

Kwa sasa Hamisa Mobetto anafanya vizuri na wimbo wake unaokwenda kwa jina la Sawa ukiwa ni wimbo wake wa tatu kutoa baada ya Madam Hero na Tunaendana.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad