Imeelezwa Ajali ya Magari Mawili iliyoua watu Zaidi ya 50 Nchini Ghana, Chanzo ni Dereva wa Moja ya Magari Hayo Alikuwa Akisinzia

Imeelezwa ajali ya magari mawili iliyoua watu zaidi ya 50 nchini Ghana, chanzo ni dereva wa moja ya magari hayo alikuwa akisinzia
Takribani watu 60 wameuawa siku ya Ijumaa baada ya mabasi mawili kugongana katika eneo la Kitampo Kusini mwa Ghana. Kwa mujibu wa polisi ajali hiyo ilitokea usiku wa kuamkia leo katika mkoa wa Bono Mashariki.


Kwa mujibu wa DW. Kamamda wa polisi Antwi Gyawu ameliambia  shirika la habari la AFP kwamba magari hayo yalikuwa yakitokea pande tofauti wakati ajali hiyo ilipotokea. Kamanda Gyawu amesema katika ajali hiyo iliyoua wato 60 moja ya mabasi hayo lilishika moto huku jingine likiharibiwa vibaya.

Mabasi hayo yanakadiriwa kuwa yalikuwa yamebeba 50 kila moja. Watoa huduma za dharura waliwasili katika eneo la tukio ikiwa ni pamoja na vikosi vya kuzima moto ili kuzima moto uliolipuka kutokana na ajali hiyo. Daktari Kwame Arhin katika wa Hospitali ya serikali ya Kitampo amesema watu 28 wamefikishwa hospitalini hapo kutokana na majeraha.

Dk. Arhin ameliambia shirika la habari la AFP kuwa watu 7 kati ya 28 waliofikishwa hospitalini hapo wako kwenye hali mbaya na wengi wamepata majeraha makubwa vichwani, na pia miili ya watu kadhaa waliofariki kwenye ajali hiyo imehifadhiwa Hospitalini hapo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad