Lipumba: Lowassa Alikuwa ni Zaidi Ya Mzigo

Lipumba: Lowassa Alikuwa ni Zaidi Ya Mzigo
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amesema kwamba japokuwa upo usemi wa kuwa mzigo mzito anapewa Mnyamwezi aubebe, mzigo wa kumnadi Lowassa ulikuwa mzito sana.

Lipumba amesema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari suala la Lowassa kuhamia CCM.

Lipumba alisema kwamba hakukubaliana na uamuzi wa washirika wenzake kumchagua Lowassa kuwa mgombea urais wa Ukawa mwaka 2015 na kwamba baada ya muda mfupi naye alitangaza nia ya kugombea urais, uamuzi ambao uliwaudhi wenzake wa Ukawa.

"Nijikute kweli Lipumba mimi nasimama jukwaani namnadi Lowassa?, Japo wanasema mzigo mzito mpe Mnywamwezi, mzigo ule ulikuwa mzito sana," alisema Profesa Lipumba.

Pamoja na hayo, Mwenyekiti huyo anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa amesema kwamba Katubu Mkuu wa Chama chao Maalim Seif hana tofauti na Lowassa kwa kuwa wote walihamia upinzani kutafuta nafasi ya kugombea urais jambo ambalo kwake amelitafsiri kama ulafi wa madaraka.

Amesema kwamba hata ndani ya CUF, Maalim Seif amekuwa akiutaka urais kwa nguvu na kusahau malengo mengine ya kitaifa ya chama, jambo ambalo amesema lingekiwezesha chama hicho kuunda Serikali ya Zanzibar.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad