Mimba Yataka Kumtoa Roho Ester Kihama

Mimba Yataka Kumtoa Roho Ester Kihama
MIMBA aliyo­nayo staa wa filamu za Kibongo, Ester Kiama ilitaka kumtoa roho baada ya kumsababishia kuumwa takribani miezi miwili bila kuinuka kitan­dani ambapo anadai alihisi kuchungulia kaburi kutokana na maumivu aliyokuwa nayo.



Akizungumza na Ijumaa Wikienda Es­ter alifunguka kuwa aliumwa sana mpaka akawa anaogopa hata kujionyesha kwa watu kutokana na alivyokonda kwani ujauzito alionao ulimsababishia kuwa na hali mbaya ingawa kwa sasa an­amshukuru Mungu anaendelea vizuri.



“Jamani nilichun­gulia kaburi kabisa, niliumwa sana lakini nafikiri ni kipindi tu cha mpito na niseme tu namshukuru Mungu kwa ku­nijaalia zawadi hii na ninamuomba sana anikamilishie safari yangu nimal­ize salama” alisema Ester Kiama.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad