Mimi, Okwi na Kagere Tuna Zawadi Yako Uwanja wa Taifa Leo

MIMI, OKWI NA KAGERE TUNA ZAWADI YAKO TAIFA LEO

KUTOA haijawahi kuwa utajiri. Ni moyo tu! Hivyo basi, mimi binafsi, Okwi na Kagere kwa kushirikiana na First 11 pamoja na subs wote wa Simba leo, tumewaandalia zawadi ya kihistoria mashabiki wa Simba na Watanzania wote.

Haikuwa rahisi kuandaa zawadi hii. Tumeidunduliza kwa muda mrefu. Leo zawadi ipo tayari kukabidhiwa kwako. Nakuhakikishia hutaondoka Uwanja wa Taifa umenuna. Utaondoka umefurahia zawadi tamu.

Unataka kujua zawadi? Ooh, zawadi ni ushindi. Zawadi ni magoli. Unataka kujua magoli ni mangapi? Idadi ya magoli ni siri yangu mimi, Okwi na Kagere. Wewe njoo Taifa leo. Boksi la zawadi tutalifungua ndani ya dakika 90.

Tukutane Kwamchina baadaye (Sorry Mwakyembe). Nakuhakikishia hatutakuangusha. AS Vita tutawapiga leo. Niamini mimi, tumekuandalia zawadi nzuri. Zawadi ya kihistoria. Zawadi ya kusimulia wajukuu zako.

Tuwe wote Taifa leo.

Ndimi Luqman MALOTO

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad