Miriam Odemba Kuwa Mstari Wa Mbele Kusheherekea Siku Ya Wanawake Duniani

Miriam Odemba Kuwa Mstari Wa Mbele Kusheherekea Siku Ya Wanawake Duniani
Mwanamitindo mkongwe ambaye anafanya kazi zake nchini Ufaransa Miriam Odemba amefunguka na kuweza wazi mipango yake ya kurudi Tanzania kwa ajili ya kusheherekea siku ya wanawake duniani.

Miriam Odemba anatarajia kuwa mmoja wa wanawake watakaohudhuria katika Onesho la Tanzanite Women Forum and Lunch linalotarajiwa kufanyika Machi 9, mwaka huu ambayo ni siku ya wanawake duniani litakalofanyika katika Hoteli ya Double Tree jijini Dar.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la ijumaa, Odemba alisema kuwa anafurahia sana kuwa mmoja wa wanawake waliopata mualiko maalum katika shughuli hiyo na kusema kuwa itakuwa ni kitu kizuri mno kwa wanawake kukutana na kujadili mambo mbalimbali pia kuangalia vitu vizuri vinavyofanywa na wanawake wenzao.

Hakuna kitu ninakipenda kama kurudi nyumbani na kukutana na wanawake wenzangu mbalimbali na kujadiliana vitu vizuri hivyo ni vyema watu wangenunua tiketi zao mapema ambazo zinapatikana sehemu mbalimbali kama Zurii House of Beuaty na Malika Designer”.



Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad