Tupunguze Lawama Kwa Diamond Kuna Wakati Yupo Sahihi Ikumbukwe Yeye ni Binadamu Pia

Nimeona leo Kidogo niwe upande wa @diamondplatnumz jamani pole kwa wale ambao nitawakwaza.
Sio kwamba @diamondplatnumz hana jema kuna mema mengi tu anayo.
Nimeona watu wakilaumu kuchelewa kwa @diamondplatnumz kushow response kwenye msiba wa Marehemu Ruge Mutahaba. Ikumbukwe Diamond alikuwa mtu wa karibu sana na Boss Ruge.
Ila ni pata taswira Diamond angefika pale mapema ingekuwaje?? Tumewahi shuhudia sehemu mbali mbali Diamond anapotokea hisia za watu zinakuwa tofauti juu yake. Mara nyingi huwa anasababisha vurugu.
Sasa angekuwepo msibani from the First Day NDO pale Bi Sandra alisema anaweza sababisha tatizo.
Hii ndio hali halisi ila pia ni mtazamo wake. Pia ikumbukwe anarinda brand yake na usalama wake pia.
Mtu kulaumu kwanini Diamond kaenda na ma Bodyguard haiji akilini. Kwahiyo watu walitaka avamiwe na umati au?? Sio poa cha kushukuru Diamond kafika na kaaga. No body is perfect.

Binafsi nimeona poa umefika eneo la tukio mengine tumwachie Mungu.
By 👉 Mdau

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad