Waziri MPYA wa Mambo ya Nje Profesa Palamagamba Kabudi Atoa ONYO Kwa Wanaoichafua Tanzania


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi, amewataka watu wanaoisema vibaya Tanzania kukaa kimya kwa sasa.

Profesa Kabudi amesema hayo leo Jumatatu Februari 4, Ikulu jijini Dar es Salaam baada ya kuapishwa kuwa waziri wa wizara hiyo na Rais John Magufuli aliyemteua juzi baada ya kufanya mabadiliko madogo ya mawaziri.

“Jana haikuwa siku nzuri kwangu niliamshwa na watu wengine kuambiwa kwamba nimeteliuwa katika nafasi hii, lakini nashukuru kwa kunipa nafasi.

“Huu si wakati wa kuisema nchi yetu, kuibeza na kuipagaza… nchi yetu ilijengwa na mwasisi Mwalimu Julius Nyerere, yeyote Mtanzania mwenye tatizo na nchi hii atutendee jambo moja tu, akae kimya.

“Tuna jambo moja tu kubwa la kujenga mahusiano na wale wanaoitakia mema nchi yetu,” amesema Profesa Kabudi.

Pamoja na Profesa Kabudi, pia Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Augustine Mahiga aliapishwa na baadhi ya Makamishna wa Jeshi la Polisi.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Agwe Mwaha.. Mlungu akutaze gwee..
    Zwalli nkutia milimo ili Baha Gwe.
    Mkulu mlungu Amtaze..
    Najisikia Faraja Sana kwa uteuzi huu

    JPJM Amechagua. Chapa ya JOGOO

    Tumo Sambamba KATIKA ujenzi na kupeleka GURUDUMU LA MAENDELEO KILA kona ya nchi yetu.. Na KILA Mzaledo namsihi Kasi yetu na mwelekeo wetu ndio huu.Vinginevyo kaa pembeni ushangilie wanaume tuko kazini.
    MWENYEZI MUNGU AKUBARIKI I SANA NA NCHI YETU PIA NA WATU WAKE.

    VIBARAKA TUNAWAJUA NA HAWANA NAFASI KATIKA NCHI YETU na Wakati wetu.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad