Amwagiwa Mafuta ya Taa na Kuchomwa Moto ili Kuondoa Mapepo

Phillipo Elias (22), mkazi wa kijiji cha Musati Wilayani Serengeti, ameunguzwa moto mwilini wakati akiombewa kanisani ili aponywe maumivu ya kichwa kwa kumwagiwa mafuta ya taa na kupigwa kiberiti kama njia ya kumfanyia ibada ya kumtoa pepo

Kwa mujibu wa maelezo yake, tukio hilo lililotokea juzi, lilifanywa na mchungaji wa Kanisa la Cag Calvary, Anna Butake ambaye amekana kumchoma moto muumini huyo akisema hajui kilichotokea hadi Phillipo akaungua kwasababu yeye alilenga kuchoma moto nguo zilizoonekana kuwa na zindiko

Philipo anasema alikwenda kwa mchungaji huyo kwa ajili ya maombi kutokana na kumfahamu akidai wanatoka wote Kigoma na kupata taarifa kuwa ana nguvu za uponyaji

Mkuu wa Polisi Wilayani Serengeti, Mathew Mgema alisema wanafuatilia na kuchunguza kwa makini tukio hilo ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad